• Login
  • Help Guide
View Item 
  •   JOOUST IR Home
  • Journal Articles
  • School of Education, Humanities & Social Sciences
  • View Item
  •   JOOUST IR Home
  • Journal Articles
  • School of Education, Humanities & Social Sciences
  • View Item
JavaScript is disabled for your browser. Some features of this site may not work without it.

Nafasi ya Fasihi Simulizi katika Karne ya 21: Tathmini ya Nyimbo za Jando za Jamii ya Wakamba.

Thumbnail
View/Open
Musembi_Nafasi ya Fasihi Simulizi katika Karne ya 21 Tathmini ya Nyimbo za Jando za Jamii ya Wakamba.pdf (238.2Kb)
Publication Date
2022-06
Author
Musembi, Naomi Nzilani
Type
Article
Metadata
Show full item record
Abstract/Overview

Fasihi simulizi ni fani hai inayotekeleza majukumu muhimu katika karne ya 21. Kama ukumbusho wa maadili ya watu, fasihi simulizi hutoa mwonoulimwengu wa jamii na kutokana nayo, hali ya maisha ya kila siku huendelezwa. Wanajamii hueleza hali yao ya maisha, utamaduni wao, maoni, mitazamo, imani na mila zao kupitia kwa utanzu huu hasa kipera cha nyimbo. Katika jamii ya Wakamba, fasihi simulizi inatumika kuelezea mielekeo na falsafa kuhusu maisha ya wanajamii. Nyimbo ni mojawapo ya fani hai ya fasihi simulizi na hubadilika kadiri hali ya maisha inavyobadilika. Mabadiliko yanayoikumba jamii kwa njia moja au nyingine hujidhihirisha katika fasihi. Maadili yalikuzwa na hata sasa yanakuzwa kupitia nyimbo hasa za jando katika jamii ya Wakamba. Katika karne hii ya 21, jamii inakumbwa na matatizo mengi hususani magonjwa yasiyo na tiba, uraibu wa dawa za kulevya, ukosefu wa kazi kwa vijana , uabudu shetani, vita vya wenyewe kwa wenyewe miongoni mwa matatizo mengine. Ili kupambana na changamoto hizi, ni muhimu kuwa na nyenzo za mawasiliano zinazoweza kutumiwa kuwafahamisha wanajamii jinsi ya kukabiliana nazo. Nyimbo za jando ni miongoni mwa njia hizi kwani kupitia kwazo, ujumbe unaweza kuwasilishwa vyema zaidi kuhusiana na namna ya kukabiliana na matatizo hayo. Hivyo basi, lengo la makala haya ni kuonesha kuwa, fasihi simulizi hasa nyimbo za jando bado zina dhima muhimu katika jamii inayobadilika.

Subject/Keywords
Nafasi ya Fasihi Simulizi .; Karne ya 21.; Tathmini ya Nyimbo; Jando za Jamii; Wakamba
Publisher
Taasisi ya Taaluma za Kiswahili Chuo Kikuu cha Dar es Salaam
Permalink
http://ir.jooust.ac.ke/handle/123456789/14246
Collections
  • School of Education, Humanities & Social Sciences [363]

Browse

All of JOOUST IRCommunities & CollectionsBy Issue DateAuthorsTitlesSubjectsThis CollectionBy Issue DateAuthorsTitlesSubjects

My Account

LoginRegister

Statistics

View Usage Statistics

Contact Us

Copyright © 2023-4 Jaramogi Oginga Odinga University of Science and Technology (JOOUST)
P.O. Box 210 - 40601
Bondo – Kenya

Useful Links

  • Report a problem with the content
  • Accessibility Policy
  • Deaccession/Takedown Policy

TwitterFacebookYouTubeInstagram

  • University Policies
  • Access to Information
  • JOOUST Quality Statement